22.11.13

Sunday, November 17, 2013

(News) MILLEN HAPPINESS MAGESE ATEMBELEA MAENDELEO YA MIRADI MTWARA

Mwanamitindo wa kimataifa wa Tanzania, Millen Happiness Magese amewataka watu binafsi na makampuni mbalimbali kujitokeza kwa wingi katika kusaidia tasnia ya elimu hasa katika maeneo yasiyopewa kipaumbele ili kuwaokoa watoto wa maeneo hayo kutotumbukia katika vitendo visivyo vya kimaadili. Rai hiyo ameitoa wakati alipotembelea miradi yake aliyoifadhili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na utengenezaji wa madawati.

Ujenzi wa madarsa unaendelea katika shule ya msingi Mjimwema iliyopo manispaa ya Mtwara ambapo mradi wa kutengeneza madawati ulikabidhiwa kwa vikundi mbalimbali vya wajasiriamali mkoani hapo kwa mpango maalum kupitia ofisi ya mkuu wa Wilaya, Mheshimiwa Wilman Ndile. Jumla ya madawati hamsini na tano (55) yenye thamani ya shilingi milioni tano yalikuwa tayari yameshatengenezwa kama walivyoahidi wajasiria mali hao wakati wakikabidhiwa kazi ya utengenezaji wa madawati hayo.


Madawati hayo yalikabidhiwa rasmi na Millen yalikabidhiwa kwa wanafunzi wa shule ya msingi Lilungu.
Kwa upande wa afisa elimu wa manispaa ya Mtwara Frola Aloys amewataka wadau wa elimu kuonesha uzalendo wa hali ya juu kwa maeneo ya Kusini mwa Tanzania huku mkuu wa shule ya msingi Lilungu Abdul Nangomwa akielezea changamoto zinazoendelea kuikumba sekta ya elimu katika shule za msingi wilayani Mtwara.


Mbali na kukabidhi madawati Millen aligtembelea ujenzi unaoendelea shule ya msingi Mjimwema na kutoa zawadi ya madaftari napenseli kwa wanafunzi hao ambapo mpaka sasa shule in mikondo mitatu ambayo ni kuanzia darasa la awali mpaka darasa la pili.


Ziara hiyo ya mrembo huyo aliyewahi kushika taji la Miss Tanzania mwaka 2001, ni mwendelezo wa shughuli za kijamii anazozifanya nchini Tanzania hasa katika kusaidia makundi yenye mahitaji maalumu na yale yasiyopewa kipaumbele.


Mwinzoni mwa mwaka huu Millen Magese alitoa kiasi cha shilingi milioni kumi na tano katika kusaidia huduma hiyo ya elimu katika manispaa ya Mtwara.

Mwisho.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:
Tabasamu PR Consultancy,
+255 754 602 674.

No comments: